TANGAZO LA KUITWA KAZINI OFISI MBALIMBALI ZA UMMA 08-03-2021






JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 
OFISI YA RAIS 
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA 
Kumb. Na. EA.7/96/01/L/64 
08 Machi, 2021


TANGAZO LA KUITWA KAZINI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anapenda kuwataarifu waombaji kazi themanini na tatu (83) wa nafasi mbalimbali serikalini ambao majina yao yapo katika tangazo hili wafahamu kuwa walifaulu usaili na kuhifadhiwa katika kanzidata (Database). Hivyo, kufuatia kufaulu kwao usaili na kupatikana kwa nafasi wazi zinazohitajika kujazwa, wamepangiwa vituo vya kazi katika ofisi mbalimbali katika Utumishi wa Umma.


Waombaji waliofaulu usaili wanatakiwa kuchukua barua za kupangiwa kituo cha kazi katika Ofisi za Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma zilizo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwenye Majengo ya Dkt. Asha Rose Migiro, Masjala ya wazi ndani ya siku saba kutoka tarehe ya tangazo hili na baada ya hapo barua ambazo hazijachukuliwa na Wahusika zitatumwa kupitia anuani zao za Posta.

Aidha, waombaji kazi waliofaulu usaili na kupangiwa kituo cha kazi wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri katika muda ambao umeainishwa kwenye barua za kupangiwa kituo cha kazi wakiwa na vyeti halisi (Originals Certificates) za masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na Mwajiri kabla ya kupewa barua ya Ajira.


Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapotangazwa.


Post a Comment

0 Comments