Azam Yakata Wanne Yasajili Wanne



Habari kutoka kunako klabu ya Azam FC zinaeleza kuwa  klabu hiyo imeamua kuachana na wachezaji wake wa 4 wa kimataifa ambao ni pamoja na washambuliaji Obrey Chirwa (Zambia) na Mpiana Mozinzi (DR Congo), kiungo Ally Niyonzima (Rwanda) na Beki Yakubu Mohammed (Ghana). 


Baada ya kuachana na wachezaji hao Azam imekamilisha usajili wa wachezaji wanne wa kimataifa ambao ni Charles Zulu (Zambia), Rodgers Kola (Zambia), Paul Katema (Zambia) na Kenneth Muguna (Kenya).

Post a Comment

0 Comments