TANGAZO LA KUAHIRISHWA KWA USAILI WA TAMISEMI KADA YA PROJECT FINANCE AND ADMINISTRATION OFFICER II



Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI anapenda kuwataarifu Waombaji Kazi waliokuwa wameitwa kwenye usaili kwa ajili ya nafasi ya Project Finance and Administration Officer II, kupitia tangazo lenye Ref.No.JA.9/259/01/4 la tarehe 15 Julai, 2021 kuwa usaili huo umeahirishwa mpaka hapo watakapotangaziwa tena/itakapotolewa taarifa nyingine

Sekretarieti ya Ajira inawaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza kutokana na kuahirishwa kwa usaili huo.


Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Sekretarieti ya Ajira
19 Julai, 2021

Post a Comment

0 Comments