TANGAZO LA KUITWA KAZINI OFISI MBALIMBALI ZA UMMA

 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS

SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA.





Kumb. Na. EA.7/96/01/L/33 16 Februari, 2021

TANGAZO LA KUITWA KAZINI

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inapenda kuwataarifu waombaji

kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili tarehe 08 – 30 Januari, 2021 kuwa

matokeo ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo ni kama yalivyoorodheshwa

katika tangazo hili. Orodha ya majina haya pia imejumuisha baadhi ya wasailiwa

waliokuwa kwenye kanzidata (Database) kwa kada mbalimbali ambao

wamepangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kupatikana.


Waombaji waliofaulu usaili wanatakiwa kuchukua barua za kupangiwa kituo cha

kazi katika Ofisi za Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma zilizopo

katika majengo ya Asha Rose Migiro yaliyomo ndani ya Chuo Kikuu cha

Dodoma (UDOM), Masjala ya wazi ndani ya siku saba kutoka tarehe ya

tangazo hili na baada ya hapo barua ambazo hazitachukuliwa na wahusika

zitatumwa kupitia anuani zao za Posta.


Aidha, waombaji kazi waliofaulu usaili na kupangiwa kituo cha kazi wanatakiwa

kuripoti kwa Mwajiri katika muda ambao umeainishwa kwenye barua za 

kupangiwa kituo cha kazi wakiwa na vyeti halisi (Originals Certificates) za

masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na mwajiri kabla ya

kupewa barua ya Ajira isipokuwa wale tu waliopangiwa Shirika la Hifadhi za Taifa

(TANAPA) utaratibu wao wa kuripoti umeainishwa katika aya inayofuata.


Waombaji kazi wote waliopangiwa kituo cha kazi Shirika la Hifadhi za Taifa

(TANAPA) wanatakiwa kuripoti tarehe 25 Februari, 2021 saa 2:00 asubuhi katika

ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi tayari kwa kuelekea katika

kambi ya mafunzo ya Jeshi Usu. Sambamba na vyeti halisi waombaji hao

waliofaulu watatakiwa kuwa na vifaa vifuatavyo vya lazima; nguo ya mazoezi

(Track Suit), Raba, Fulana, Bukta, Begi la mgongoni (Day Pack/Rucksack) na

Soksi jozi za kutosha.


Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili watambue kuwa

hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine

nafasi za kazi zitakapotangazwa.

Bofya hapa kupakua PDF

Post a Comment

0 Comments