TANGAZO KUITWA KWENYE USAILI SHUWASA

 

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA), anapenda kuwataarifu waombaji kazi waliotuma maombi ya kujaza nafasi wazi za Taasisi hizo, kuwa usaili utafanyika tarehe 24 na 25 Mei, 2021 na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo. Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:- 


i. Usaili utafanyika tarehe 24 na 25 Mei, 2021 kama ilivyoainishwa kwenye tangazo hili; 

ii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa barakoa; 

iii. Kila msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi; 

iv. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria; 

v. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada nakuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji; 

vi. Wasailiwa watakaowasilisha “Testimonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati za matokeo za kidato cha IV na VI (form IV and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI; 

vii. Kila msailiwa atajigharamia kwa chakula, usafiri na malazi; 2 

viii. Kila msailiwa azingatie tarehe na mahali alipopangiwa kufanyia usaili; 

ix. Kwa waombaji kazi waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika (TCU na NECTA); 

x. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo, hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika; 

xi. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti vyao halisi vya usajili pamoja na leseni za kufanyia kazi. 

xii. Wasailiwa wote wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na kunakili namba ya mtihani kwa kuwa namba hizo hazitatolewa siku ya usaili.



Post a Comment

0 Comments