Mangalo Athibitisha Kuwa na Mazunguzo na Yanga



 BEKI wa Kati na Nahodha wa Biashara United, Abdulmajid Mangalo, amesema kuwa Yanga bado wapo kwenye mazungumzo na uongozi wake. Mangalo amekuwa akihusishwa na Simba na Yanga tangu usajili wa dirisha kubwa msimu huu ufunguliwe.

Kwa upande wa beki huyo anasema hana ushabiki wowote na ataenda popote watakapoonyesha kumhitaji. Mangalo amesema kuwa:

“Nasikia Yanga wapo kwenye mazungumzo na uongozi wangu na mimi nitaenda pale ninapohitajika. “Kwa sasa naweka akili yangu kwenye michuano ya Cecafa Chalenji huku Ethiopia, nitakaporejea nitajua kila kitu,” alisema Mangalo

Post a Comment

0 Comments